Breaking News

Wednesday

AGNES MASOGANGE AKAMATWA NA MADAWA YA KULEVYA AFRIKA KUSINI.

Mabinti wa wili wanaodaiwa kuingiza shehena ya dawa za kulevyazenye thamani ya zaidi ya bilioni 6.8 nchini Afrika Kusini wakitoka Tanzania.
Akizingumza na mwandishi wetu jana,kamanda wa polisi ktengo cha kupambana na dawa za kulevya,  Geofrey Nzoa, alisema hajafahamika wanawake hao wanatoka mikoa gani.
Kamanda Nzoa aliwataja wanawake hao kua ni Agnes Jerald(MASOGANGE) ambaye alisema hajapiga hesabu za umri wao, ili alizaliwa mwaka 1988 kwa maana hiyo ana umri wa miaka 25 na Melisa Edward ambaye alisema amezaliwa mwaka 1989 kwa maana hiyo ana umri wa miaka 24. Wawili hao bado waendelea kuhojiwa na polisi wa Afrika kusini.
Alisema Jeshi la  polisi Nchini kwa upande wake linaendelea kufanya uchunguzi kubaini kama dawa hizo walitoka nazo wapi na pia linawasaka watu ambao watakua ndiyo amiliki wa dawa hizo.
Jumapili iliyopita mtandao huu ulipata taarifa za kukamatwa kwa dawa za kulevya aina ya crystal methamphetamine zenye thamani hiyo nchini Afrika kusini wakati zikisafirishwa kutoka Tanzania.
Taarifa hizo zilionyesha kuwa wanawake wawili walikamatwa katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Oriver Tambo uliopo eneo la Kempton Park siku ya Ijumaa wiki iliapita wakitokea Tanzania.
Wanawake hao walikamatwa na maofisa wa mamlaka ya  mapato ya Afrika kusini wakiwa na masanduku sita ambayo yalipokaguliwa yalikutwa na takribani kilo 150 za dawa hizo ambazo pia zinajulikana kama “TIK” zikiwa na thamani ya bei ya mtaani ya Randi milioni 42 sawa n ash. Bilioni 6.8
Baada ya kukamatwa na dawa hizo  wanawake hao walikabidhiwa polisi. Tukio hilo linatoka takribani wiki moja baada ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, Juni 28 mwaka huu kutangaza kuwa tatizo la dawa za kulevya hivi sasa ni janga nchini.


Alisema kumekua na wimbi kubwa la watanzania wanaojiiongiza katika biashara za  haramu ya madawa ya kulevya ndani na nje ya nchi  na kwamba katika  cha miaka mitano iliopita watuhumiwa 10799 walikamatwa kwa kujihusisha na dawa hizo.
Pia alisema katika kipindi hicho Watanzania 240 walikamatwa katika nchi za Brazil, Pakistan na Afrika Kusini, na hivyo kuharibu taswira ya nchi na kusababisha Watanzania wasio na hatia kupata usumbufu na masharti magumu wanapotaka kusafiri kwenda nchi mbalimbali duniani.
Panda alisema mwaka huu pekee kumekuwa na ukamataji mkubwa wa dawa za kulevya katika eneo la kimataifa la Bahari ya Hindi karibu na Tanzania.
Alisema hivi sasa mikate maandazi na askrimu zinazouzwa kwenye shule za msingi zimewekwa dawa za kulevya.
Alisema vitendo hivyo vinafanya vijana wengi wa shule za msingi na hata sekondari kuwa na tabia za ajabu ikiwemo kuingia darasani wakiwa na kiatu kimoja mguuni, mkufu wenye nyembe na kidani chenye nyembe kifuani.
Maelezo kwa hisani ya NIPASHE
Share:

Related Posts:

0 comments:

Post a Comment

Chapisho Lililoangaziwa

WEDDING PARTY PHILLIPO AND LUSIO

PHILLIPO & LUSIO WEDDING PARTY: STILL PICTURE, VIDEO SHOOTING MC & MUSIC BY MC SIMBA COMPANY 0715 501 059 ...

Jumla ya Mara Iliyotazamwa

67145
Powered by Blogger.

Pages