Shabiki mmoja raia wa Vetnam jana alifanya kitendo cha ajabu baada ya kukimbia sambamba na basi lilowabeba wachezaji wa Arsenal kwa takribani maili 3.
Katika kulikimbilia basi hilo alikutana na vigingi tofauti lakini
kijana yule wa kivetnam hakukata tamaa ya kulifikia basi la Arsenal na kuwaona wachezaji wa timu aipendayo.
Baada ya kulikimbiza basi hilo kwa muda mrefu hatimaye kijana
huyo alipata msaada kutoka kwa mwenye pikipiki na kuufikia
mlango wa basi hilo na wachezaji wa Arsenal wakamfungulia
mlango kisha kumpokea kwa furaha.
Kijana huyo alitimiza ndoto yake baada ya kupiga picha na
wachezaji wote pamoja na kocha Arsene Wenger.
0 comments:
Post a Comment