Breaking News

Friday

MRISHO NGASSA AIDHINISHWA KUICHEZEA YANGA "SHARTI LA KUILIPA SIMBA MILLIONI 45".

Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu 
Tanzania (TFF) imepitia usajili wa wachezaji wa klabu za Ligi Kuu ya 

Vodacom na kumuidhinisha Mrisho Ngasa kuchezea timu ya Yanga
 baada ya kukamilisha usajili wake.
Hata hivyo, Kamati hiyo chini ya Mwenyekiti wake Alex Mgongolwa
 imebaini kuwa Ngasa alisaini mkataba mwingine Simba (katika kipindi
 ambacho alikuwa na mkataba na Azam) ambapo anatakiwa kurejesha 
fedha alizopokea (sh. milioni 30) pamoja na fidia ya asilimia 50
 (sh. milioni 15) ya fedha hizo kwa Simba.
Kamati pia imemfungia mechi sita za mashindano (kuanzia mechi ya 
Ngao ya Jamii), na anatakiwa awe amelipa fedha hizo ndani ya kipindi
hicho cha kukosa mechi hizo. Akishindwa, hataruhusiwa kucheza hadi 
atakapolipa fedha hizo.Na Shaffih dauda
Vilevile Kamati imepitia pingamizi zote zilizowasilishwa kuhusu 
usajili wa wachezaji, kukatiza mikataba ya wachezaji na kuzitaka 
klabu husika ziwe zimetatua masuala hayo hadi Alhamisi 
(Agosti 22 mwaka huu).
Kwa upande wa wachezaji wa kigeni, Kamati imeagiza wasiruhusiwe 
kucheza hadi watakapopata Hati za Uhamisho wa Kimataifa (ITC)
 pamoja na vibali vya kufanya kazi nchini (work permits).
Kamati hiyo itakutana tena Ijumaa (Agosti 23 mwaka huu) ili
 kupata ripoti za pingamizi ilizoagiza ziwe zimefanyiwa kazi hadi 
Agosti 22 mwaka huu na kutoa uamuzi kwa pande ambazo 
hazikuafikiana.
source:jumamtanda.

Share:

0 comments:

Post a Comment

Chapisho Lililoangaziwa

WEDDING PARTY PHILLIPO AND LUSIO

PHILLIPO & LUSIO WEDDING PARTY: STILL PICTURE, VIDEO SHOOTING MC & MUSIC BY MC SIMBA COMPANY 0715 501 059

Jumla ya Mara Iliyotazamwa

Powered by Blogger.

Pages