Breaking News

Wednesday

JEMBE LA UKWELI, AMRI ATHMANI KIEMBA ASAINI MKATABA MPYA NA SIMBA KWA DAU LA SH. MILIONI 35.



Baada ya kuzagaa kwa taarifa kuwa kiungo nyota wa klabu ya Simba na timu ya taifa ya Tanzania, Amri Athman Kiemba “Jembe la kulimia katika kokoto” kuwa alikuwa katika rada za Yanga ambao walitaka kuwaliza Simba kwa kumsainisha mkataba, hatimaye ubishi waashi baada ya nyota huyo kusaini mkataba na mnyama kwa kitita cha shilingi milioni 35.
Hatimaye mazungumzo baina ya Klabu ya Simba na mchezaji Amri Kiemba yamemalizika kwa pande hizo mbili kukubaliana kuongeza mkataba mpya, hivyo kuwaondolea presha mashabiki wa Simba na Viongozi walikuwa na hofu ya kupigwa bao na Yanga.
Mchana wa leo Simba ilikuwa kwenye jitihada nzito kuhakikisha inamzuia Kiemba kusaini Yanga kwa kumpa ofa nono ya mkataba mpya, Kiemba alikuwa akihitaji kiasi cha millioni 38 ili asaini msimbazi lakini baada ya mazungumzo marefu Kiemba amekubali kusaini kwa kiasi cha millioni 35 kwa miaka miwili.
Pia Kiemba atakuwa analipwa mshahara wa millioni 2 kwa mwezi. Alisaini mkataba huo mbele ya kaimu makamu mwenyekiti  Mzee Kinesi.
                                          *ASANTE KWA KUTEMBELEA BLOG YETU*

Share:

Related Posts:

0 comments:

Post a Comment

Chapisho Lililoangaziwa

WEDDING PARTY PHILLIPO AND LUSIO

PHILLIPO & LUSIO WEDDING PARTY: STILL PICTURE, VIDEO SHOOTING MC & MUSIC BY MC SIMBA COMPANY 0715 501 059 ...

Jumla ya Mara Iliyotazamwa

67157
Powered by Blogger.

Pages