Baada ya kuzagaa kwa taarifa kuwa kiungo nyota wa klabu ya Simba na timu
ya taifa ya Tanzania, Amri Athman Kiemba “Jembe la kulimia katika kokoto” kuwa
alikuwa katika rada za Yanga ambao walitaka kuwaliza Simba kwa kumsainisha
mkataba, hatimaye ubishi waashi baada ya nyota huyo kusaini mkataba na mnyama
kwa kitita cha shilingi milioni 35.
Hatimaye mazungumzo baina ya Klabu ya Simba na mchezaji Amri Kiemba
yamemalizika kwa pande hizo mbili kukubaliana kuongeza mkataba mpya, hivyo
kuwaondolea presha mashabiki wa Simba na Viongozi walikuwa na hofu ya kupigwa
bao na Yanga.
Mchana wa leo Simba ilikuwa kwenye jitihada nzito kuhakikisha inamzuia
Kiemba kusaini Yanga kwa kumpa ofa nono ya mkataba mpya, Kiemba alikuwa
akihitaji kiasi cha millioni 38 ili asaini msimbazi lakini baada ya mazungumzo
marefu Kiemba amekubali kusaini kwa kiasi cha millioni 35 kwa miaka miwili.
Pia Kiemba atakuwa analipwa mshahara wa millioni 2 kwa mwezi. Alisaini
mkataba huo mbele ya kaimu makamu mwenyekiti Mzee Kinesi.
0 comments:
Post a Comment