Breaking News

Tuesday

MBUGE MAHAKAMINI KWA UCHOCHEZI



Mbunge wa jimbo la Mtwara, eneo ambalo limekumbwa na vurugu hivi karibuni kusini mwa Tanzania amefikishwa mahakamani  akituhumiwa kwa makosa ya uchochezi wa vurugu zilizo sababisha vifo vya watu watatu mwezi uliopita.
Hasnain Murji pamoja na watuhumiwa wengine 91 wamefikishwa kwenye mahakama ya wilaya ya Mtwara.
Kwa muda huu baadhi ya watuhumiwa wamepata dhamana huku wengine wakiendelea na taratibu za kukamilisha udhamini, wakati Mbunge huyo akisubiri kupandishwa kizimbani na kusomewa mashtaka yanayo mkabili.
Wananchi waliofika mahakamani kwa ajili ya kusikiliza kesi zinazowakabili ndugu na jamaa zao wamelalamikia utaratibu wa kuwazuwia kuingia mahakamani hapo.
Mbunge huyo wa Chama kinacho tawala nchini humo CCM, alikamatwa na kushikiliwa na jeshi la Polisi mkoani humo siku ya Jumamosi.
Idadi kubwa ya wananchi wa Mtwara wamekuwa katika mvutano mkali na Serikali yao ambayo imekusudia kujenga bomba la kusafirisha gesi asilia inayopatikana mkoani humo hadi Dar es Salaam, Hatua inayopingwa na wananchi hao ambao wanadai gesi hiyo isisafirishwe na kupelekwa popote.

                 *ASANTE KWA KUTEMBELEA BLOG YETU*

Share:

Related Posts:

0 comments:

Post a Comment

Chapisho Lililoangaziwa

WEDDING PARTY PHILLIPO AND LUSIO

PHILLIPO & LUSIO WEDDING PARTY: STILL PICTURE, VIDEO SHOOTING MC & MUSIC BY MC SIMBA COMPANY 0715 501 059 ...

Jumla ya Mara Iliyotazamwa

67151
Powered by Blogger.

Pages