Breaking News

Friday

RASIMU YA KATIBA YAVURUGA MIPANGO YA URAIS 2015 .... RIPOTI KAMILI NA MIPANGO YAO MIPYA HII HAPA


Mapendekezo yaliyotolewa katika Rasimu ya Katiba Mpya na Tume ya Marekebisho ya Katiba yamewavuruga wanasiasa ambao tayari walikuwa wamejipanga kwa ajili ya kuwania urais katika Uchaguzi Mkuu wa 2015, Mwananchi limebaini.
Tangu juzi Mwenyekiti wa Tume hiyo, Jaji Joseph Warioba alipotangaza rasimu hiyo, kumekuwa na wasiwasi mkubwa sasa kwamba mipango ya urais wa 2015 itavurugika ikiwa mapendekezo hayo yatapitishwa.
Tishio kubwa katika rasimu hiyo ni pendekezo la kuwapo kwa Serikali ya tatu hali ambayo inatafsiriwa na baadhi ya wanasiasa kwamba inaondoa nguvu ya Rais yeyote; awe wa Jamhuri ya Muungano, Zanzibar au Tanzania Bara.
Habari za kuaminika zilizopatikana kutoka ndani ya kambi za vyama vya CCM na Chadema zinaeleza kuwa wale waliokuwa wakifikiria kuwania nafasi hiyo wameingiwa na wasiwasi.
Kadhalika, suala la umri wa kuwania urais kubakia miaka 40 pia linaonekana kuwagusa waliowahi kutangaza kutaka nafasi hiyo ya juu ya uongozi wa nchi kabla ya mapendekezo ya tume.
Katika suala la urais, wanasiasa wenye nia hiyo wanauona uongozi wa Jamhuri ya Muungano kuwa ni kama hauna nguvu tena kutokana na kushughulikia mambo machache, lakini wakati huohuo wanauona urais wa Tanzania Bara kwamba hauna mamlaka kamili ya kuwawezesha watambuliwe nje ya nchi.
Tume ya Marekebisho ya Katiba imependekeza mambo saba tu yawemo chini ya Serikali ya Muungano kati ya 22 ya sasa. Yanayopendekezwa ni Ulinzi na Usalama, Katiba na mamlaka ya Jamhuri ya Muungano, mambo ya nje, sarafu na Benki Kuu, uraia na uhamiaji, usajili wa vyama vya siasa, ushuru wa bidhaa na mapato yasiyo ya kodi yatokanayo na Muungano.
Ndani ya CCM
Makundi mbalimbali yanayowania urais ndani ya CCM inaaminika hayajafurahishwa na mapendekezo ya rasimu ya kutaka Serikali tatu.
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI
Share:

Related Posts:

0 comments:

Post a Comment

Chapisho Lililoangaziwa

WEDDING PARTY PHILLIPO AND LUSIO

PHILLIPO & LUSIO WEDDING PARTY: STILL PICTURE, VIDEO SHOOTING MC & MUSIC BY MC SIMBA COMPANY 0715 501 059 ...

Jumla ya Mara Iliyotazamwa

67154
Powered by Blogger.

Pages