Breaking News

Sunday

UGANDA YA FUFUA MATUMAINI YA KWENDA BRAZIL


Timu ya Taifa ya Soka ya Uganda, imeilaza Liberia kwa bao moja kwa bila na kuimarisha matumaini yake ya kufuzu kwa kombe la dunia mwaka ujao nchini Brazil, katika mechi kali iliyochezwa mjini Kampala.
Kufuatia ushindi huo Uganda Cranes sasa imepanda hadi nafasi ya pili katika kundi J na alama 5 nyuma ya vinara wa kundi hilo Senegal ambao wanachuana na Angola.
Uganda sasa imesalia na mechi mechi mbili na imepangiwa kuchuana na Angola tarehe 15 mwezi huu kabla ya kupepetana na Senegal tarehe 6 Septemba mwaka huu katika uwanja wa Leopold Senghor.
Uganda ni sharti ishindi mechi zake zilizosalia ili kuwa katika nafasi nzuri ya kufuzu kwa fainali hizo zitakazoandaliwa nchini Brazil Januari mwakani.
Katika mechi zingine za kufuzu kwa Fainali hizo, Zambia wameilaza Lesotho kwa magoli 4-0 nayo Botswana wakalemewe nyumbani kwao na Ethiopia kwa kufungwa magoli 2-1

Share:

Related Posts:

0 comments:

Post a Comment

Chapisho Lililoangaziwa

WEDDING PARTY PHILLIPO AND LUSIO

PHILLIPO & LUSIO WEDDING PARTY: STILL PICTURE, VIDEO SHOOTING MC & MUSIC BY MC SIMBA COMPANY 0715 501 059 ...

Jumla ya Mara Iliyotazamwa

67162
Powered by Blogger.

Pages