MSHAMBULIAJI Gonzalo Higuain yuko njiani kutua London kukamilisha uhamisho wake wa Pauni Milioni 22 kutua Arsenal.
The Gunners ipo karibu kumsajili Muargentina huyo na wapo katika hatua za mwisho za kuthibitihsa fili dilo.
Higuain, ambaye ameambiwa yuko huru kuondoka Real Madrid anatarajiwa kutua London leo kwa mazungumzo.
Karibu yatatimia: Jinsi gani Higuain ataonekana akiwa katika uzi wa Arsenal, hii ni picha ya 'magumashi'
Baba yake ameonyesha daliliza kukamilisha kwa dilo hilo.
"Hatutajadiliana na klabu yoyote bila ya ruhusa ya klabu inayotaka kumuuza,"alisema Higuain kuiambia TuttoMercato.
"Tuna ruhusa [kutoka Madrid] na ni matumaini karibuni tutamuona mwanangu katika Ligi Kuu England.’
Arsenal imekamilisha usajili wa mshambuliaji kinda Mfaransa, Yaya Sanogo Jumatatu wiki hii.
Johan Djourou na Vito Mannone tayari wametolewa kwa mkopo na kuuzwa, wakati Arsene Wenger ameripotiwa kutaka kuwasajili Wayne Rooney, Marouane Fellaini na Lars Bender
0 comments:
Post a Comment