
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akihojiwa na Mtangazaji, Adesewa Josh kutoka Channels TV ya nchini Nigeria wakati wa mkutano wa wake wa Marais wa nchi zaa Afrika unaofanyika katika hoteli ya Serena hapa Dar es Salaam tarehe 3.7.2013.


Baadhi ya washiriki wa mkutano wa wake wa marais wa Afrika wakisikiliza hotuba ya Rais Jakaya Kikwete alipohutubia mkutano huo tarehe 3.7.2013.

Rais Jakaya Kikwete akihutubia mkutano wa siku mbili wa wake wa marais wa Afrika unaofanyika katika hoteli ya Serena hapa Dar es Salaam.

Rais Jakaya Kikwete akiwa na Rais Mstaafu wa Marekani Mheshimiwa George Bush na mke wake Mama Laura Bush pamoja na Mama Salma Kikwete wakiangalia igizo lililokuwa linafanya na kikundi cha Tanzania House of Talent wakati wa mkutano wa wake wa marais wa Afrika unaofanyika katika hoteli ya Serena tarehe 3.7.2013.

Rais Jakaya Kikwete akiwa na mgeni wake Rais Mstaafu wa Marekani Mheshimiwa George Bush wakiwa katika picha ya pamoja na wake wa marais wa Afrika na wana kikundi cha Tanzania House of Talents mara baada ya kufanya igizo kwenye mkutano wao kwenye hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam tarehe 3.7.2013.
Picha na:mwanahabari wetu
**ASANTE KWA KUTEMBELEA BLOG YETU**
0 comments:
Post a Comment